Articles

Mambo 10 ambayo kijana hutakiwi kuyafanya

Image
 💝 (1). Kuchagua Kazi. Ni vigumu kupata Kazi ukiwa nje ya Kazi. Fanya Kazi uliyoipata upate Kazi unayoitaka. (2). Kuchagua sehemu ya kuishi /kufanyia Kazi. Maisha ni safari ndefu, maisha ni popote, si lazima kukaa mjini. Hauwezi kujua ni sehemu gan iliyobeba mafanikio yako. Chagua sehemu yenye FURSA na si yenye MAGHOROFA. (3). Kuishi bila kuwa na malengo. Maisha si bahati mbaya au nzuri. Maisha ni mipango, Maisha yanaongozwa na malengo. Vile ulivyo leo ni matokeo ya jinsi ulivyopanga jana, na vile unavyoishi leo ndivyo kesho yako itakavyokuwa. PANGA KESHO YAKO SASA. (4). Maisha Ya kuiga. Maisha yako si ya mwenzako, na ya maisha ya mwenzako si ya kwako. Si kila ukionacho ni lazima ufanye, chagua kipi cha kufanya na kipi cha kuacha. Kupitwa na jambo wakat mwingine sio USHAMBA bali ni BUSARA. (5). Kuishi juu ya kipato chako. Ishi kulingana na vile ulivyonavyo na si usivyonavyo. Kuwa na Busara katika MATUMIZI uepukane na MADENI yasiyo na ULAZIMA. RIDHIKA NA VILE ULIVYONAVYO. (6).Kuishi bi

Jinsi ngono inavyo angamiza maisha ya vijana

Image
  Zamani soko la ngono lilikuwa likisimamiwa na wazee na jamii yote kwa ujumla . Ilikuwa vigumu sana kwa vijana kujiingiza kwenye mahusiano kabla ya ndoa kwa sababu jamii iliweka mipaka kwenye mahusiano . Mipaka ya mahusiano mara nyingi iliendana na mahitajio ya kiimani, hii ilipelekea kukubalika kwa utaratibu kwamba ili kijana kushiriki ngono ilimlazimu kuingia kwenye ndoa. Inawezekana ndio sababu likaitwa  tendo la ndoa , yaani linalofanyika ndani ya ndoa pekee. Katika dunia ya leo,  soko la ngono limekosa msimamizi halisi . Mamlaka za kidunia zimeingilia kati kufuatia  mahitajio ya wanawake kutaka usawa kwenye ngono  (sexual revolution) na kuweka uwanja sawa wa biashara hii. Matokeo yake wazee hawana tena uwezo wa kusimamia soko hili ili mnunuzi na muuzaji wawe wamekidhi vigezo vya kiasili, badala yake kila mtu anaingia sokoni vile atakavyo. Hatari kubwa kwa vijana Kwa kuwa leo hii hakuna anayesimamia soko la ngono, jamii imekubali kwamba  hakuna tena umri sahihi wa kijana kuingia k

Anza biashara yako kwa mtaji mdogo

Image
  Nimekuwa nikipokea maoni mengi sana kutoka kwa wasomaji wakitaka ushauri kuhusu biashara gani wanaweza kufanya kwa mtaji kidogo walioko nao. Huenda na wewe umeshajikuta kwenye njia panda kama hii na kushindwa kujua ufanye nini. Leo utajua ni kipi cha kufanya katika hali kama hii. Kabla ya kuendelea hebu tuone baadhi ya maoni ya wasomaji wenzetu waliotuandikia; Nimemalza chuo mwaka jana sijaajiriwa, nina ndoto za kujiajiri lakini mpaka sasa nmefanifakiwa kupata lak 3 so sjui nianzie wapi na nianze na lipi kwa huu mtaj maana kukodi frem tu ni elf 30/mwez na wanahtaj miez 6 Nahitaji kufanya biashara, na nimeshaanda mtaji kiasi kama cha millioni 2 . Tatizo langu nashindwa nifanye biashara gani na nianze vp? Naomba msaada wako. Ni mradi, miradi gani nianzise kwa mtaji wa laki mbili? Hayo ni baadhi tu ya maoni mengi ambayo nimepokea kuhusu changamoto ya biashara gani ya kufanya hasa mtu anapokuwa na mtaji kidogo. Kitu kikubwa ambacho mpaka sasa nimejifunza kutokana na mawasialiano na watu