Articles

Usikimbilie Kujenga Kabla Hujawa Na Uhakika Wa Kipato.

Image
  Karibu tena kwenye kipengele hiki cha   ushauri wa changamoto   mbalimbali zinazotuzuia kufikia mafanikio makubwa. Mpaka sasa tumeshajadili changamoto nyingi na kujifunza kupitia changamoto za wengine bonyeza hayo maandishi. Katika moja ya changamoto ambazo tumewahi kujadili ni kuhusu kujenga au kutokujenga hasa pale ambapo mtu anakuwa hana kipato cha uhakika. Katika makala; USHAURI;  Kipi bora kujenga au kuwekeza kwenye biashara ? Tulijadili kwa kina kuhusu kipi bora kati ya kujenga au kuwekeza fedha hiyo kwenye biashara. Hivi karibuni msomaji mwenzetu ametupa maoni yake akieleza changamoto ambayo inamkabili. Changamoto hii ni sawa kabisa na ile tuliyojadili ya kuhusu kujenga au kuwekeza kwenye biashara, ila changamoto yake imeenda mbali kidogo hivyo nimeona ni bora tuijadili tena. Kabla hatujaingia kwenye ushauri naomba nikupe nafasi ya kusoma kile ambacho tumeandikiwa na msomaji mwenzetu; Ndugu yetu huyu ameuliza maswali mawili ya muhimu sana kwake yanayompatia ...

Jinsi ya kutoka kuajiriwa mpaka kujiajiri

Image
  Kununua uhuru wa kazi na hata maisha, yaani kutoka kuwa mwajiriwa mpaka kujiajiri mwenyewe na hatimaye kuweza kuwaajiri wengine ni mpango wa watu wengi sana. Japo ni wachache sana wanaoweza kutimiza mpango huu kwa sababu sio kitu rahisi kufanya kama ilivyo rahisi kusema. Unahitaji kudhamiria kweli, unahitaji kujitoa kweli na pia unahitaji kufanya tofauti sana na vile ulivyozoea kufanya au vile ambavyo kila mtu anafanya. Leo katika kipengele hiki cha  ushauri wa changamoto  tutajadili changamoto ambazo zinawazuia watu wengi kuweza kununua uhuru wao na hatua gani za kuchukua ili uweze kununua uhuru wako. HAKIKISHA UNASOMA KITABU HIKI, BONYEZA KUKIPATA   Kabla hatujaangalia ni kipi cha kufanya, naomba tupate maoni kutoka kwa msomaji mwenzetu ambaye anapitia changamoto hii. Na maoni ya leo ni marefu kidogo hivyo yasome kwa umakini ili tuweze kwenda vizuri. Habari mkuu, Mimi nafanya kazi na nina familia sasa majukumu yamekuwa mengi na kipato hakitoshi kabisa na nina pla...

Tengeneza ujana wako

Image
  Tafadhali tafakari maswali haya – una maarifa ya kitaalamu yenye thamani sana kutokana na maisha yako ya ujana: Ulipata uzoefu gani katika mabadiliko yako ya kutoka utotoni na kuwa kijana? Ni kwa vipi uhusiano wako wa kijamii na kundi rika ulibadilika? Ulipata uzoefu gani wa mabadiliko yako ya kimwili? Ulipata uzoefu gani wa mabadiliko yako ya kihisia? Ni kitu gani kilikufanya ukasirike au uone aibu? Ni kwa jinsi gani tabia, mwenendo na mitazamo dhidi ya wazazi wako vilibadilika? Nini ambacho wazazi wako na watu wazima wengine walifanya kukusaidia – nini walifanya ambacho hakikuwa cha msaada? Je, uliwahi kupata mitanziko kati ya kuwa mtiifu kwa wazazi wako na kutaka kuwa na maisha huru? Tafadhali eleza. Kama hitimisho: Nini kilikuwa changamoto kubwa kwako kama kijana? Tafadhali andika mawazo hayo kama ujuzi na uzoefu wako binafsi katika kumsaidia kijana wako anayebalehe unayemlea. UKUAJI WA JUMLA NA MAJUKUMU WAKATI WA KUSHUGHULIKA NA VIJANA BALEHE Kwa ujumla umri wa ujana wa mtot...

Jinsi ya Kufanikisha Ujana Wako

Image
  WAKAZI wa nchi moja barani Ulaya waliombwa wachague kati ya mambo matatu: urembo, utajiri, au ujana. Wengi walichagua ujana. Naam, watu wa kila rika huona miaka ya utineja na miaka ya mapema ya 20 kuwa wakati wa pekee maishani. Na kila mtu anataka vijana wafanikiwe wanapokuwa watu wazima. Lakini jinsi gani? Je, Biblia inaweza kusaidia? Kwa wazi jibu ni ndiyo. Acheni tuchunguze sehemu mbili ambazo Neno la Mungu linaweza kutoa msaada wa pekee unaoweza kuwasaidia vijana hasa kuliko watu wa rika lolote. Kupatana na Wengine Ripoti inayoitwa  Jugend 2000  ni uchunguzi unaofanywa kuhusu mtazamo, maadili, na tabia ya vijana zaidi ya 5,000 katika sehemu nyingi nchini Ujerumani. Uchunguzi huo unafunua kwamba vijana wanapojifurahisha—kama vile wanaposikiliza muziki, wanapocheza, au wanapotembea-tembea tu—karibu wakati wote wanakuwa na watu wengine. Labda vijana ndio hupenda sana kuwa pamoja na marika wao, kuliko watu wa rika lolote. Kwa sababu hiyo, ni wazi kwamba mojawa...

MJUWE MWANAMKE ANAYE KUPENDA ILA ANASHINDWA KUKUAMBIA

Kumekuwa na imani potofu kwa wanawake kwamba hawawezi kumwambia ukweli mwanaume anampenda kwanza mpaka mwanaume aanze lakini ukweli usiopingika ni kwamba wao pia hupendi na mara nyingi wao wakianza kupenda hupenda kweli kufikia stage hata ya kuhisi kuumwa. Hizi ni dalili za mwanamke anaekupenda ila anagoma kukwambia tu. 1. KUKUTEGA ILIKUJUA THAMANIYAKE KWAKO Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama unampenda na kumthamini au la mfano wa mambo hayo ni kama kujifanya anaumwa na kauangalia respond yako kwake ni kiasi gani unamjali na kiasi gani utahangaika kwa ajili yake. 2.HUWA ANAPENDA KUKUGUSA SEHEMU YAKO YA MWILI. Haoni aibu kugusa sehemu ya mwili wako. Msichana anayependa haoni aibu kukushika mkono ama kukutomasa au hata kukumbatia.Kwa kufanya hivyo hujua kuwa kwa asilimia kubwa hisia za kushikana kwenu kutamrahishishia kazi ya kuwa na wewe. 3. KUPENDA KUCHEKA TENA MUDA MWINGINE KWA NGUVU Kucheka kwa nguvu hata kwa kitu kisicho chekesha endapo wewe umezungumza. Mara nyingi ataonesh...